Wednesday 14 December 2016

USAFI WA MAZINGIRA KATIKA HOSTELI ZA CHUO CHA UANDISHI WA HABARI NA UTANGAZAJI ARUSHA



Wanafunzi wa chuo cha uandishi wa  habari na utangazaji Arusha wakiwa katika usafishaji wa mazingira katika hosteli za chuo hicho mapema hii leo
Wanafunzi hao wametoa wito kwa jamii nzima kusafisha mazingira yanayowazunguka ili kuepukana na magonjwa mbalimbali ya mlipuko na kuungana na kauli ya Raisi ya usafishaji  mazingira
Hata hivyo wanafunzi hao wameuomba uongozi wa chuo kuwapatia vifaa vitakavyo wawezesha kusafisha mazingira yanayowazunguka kwa wakati swala ambalo pia litasaidia taaluma ya chuo hicho  kuongezeka kiwango
Aidha wananchi wanao zizunguka hosteli za chuo hicho wamewapongeza wanafunzi hao kwa jitihada zao katika usafishaji wa mazingira ya eneo hilo
                    ‘kwa kweli na wasifu wanafunzi wa chuo hichi kwani wamekuwa mfano mzuri kwa jamii hususani kata hii ya olasiti kwa jitihada za usafishaji  na utunzaji mzuri wa mazingira yao’ Alisema Bi Salma Rashidi ambaye ni mmoja kati ya  wakazi wa eneo hilo